Job 8:3-7


3 aJe, Mungu hupotosha hukumu?
Je, Mwenyezi hupotosha kile kilicho haki?

4 bWatoto wako walipomtenda dhambi,
aliwapa adhabu ya dhambi yao.

5 cLakini ukimtafuta Mungu,
nawe ukamsihi Mwenyezi,

6 dikiwa wewe ni safi na mnyofu,
hata sasa atainuka mwenyewe kwa niaba yako,
na kukurudisha katika mahali pako pa haki.

7 eIjapokuwa mwanzo wako ulikuwa mdogo,
lakini mwisho wako utakuwa wa mafanikio.

Copyright information for SwhKC